MAWASILIANO YA BLOG

KWA MAONI NA USHAURI WASILIANA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO KWA SIMU NAMBA 0764 143 977 AU E-MAIL: habarigeita@gmail.com

Tuesday 2 February 2016

MHESHIMIWA SAMIA SULUHU MAKAMU WA RAIS AZINDUA WODI YA WAGONJWA WA DHARULA, MRADI WA MAJI, KIKUNDI CHA USHONAJI CHA AKINA MAMA NA VIJANA , MITAMBO YA UJENZI WA BARABARA MKOANI GEITA.

Mheshimiwa Samia Suluhu Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akikabidhi Mashine ya Echo Mganga Mkuu wa Mkoa wa Geita Joseph Kisala alipotembelea Hospitali hiyo na kuzindua wodi ya wagonjwa dharula na wodi ya watoto. Mashine hiyo ni moja kati ya vifaa vya kisasa ambavyo vimewekwa katika Hospitali hiyo na serikali kwa lengo la kuhakikisha kwamba wananchi wanapata huduma bora za Afya na kwa wakati. Aidha katika ziara hiyo Makamu wa Rais alizindua mitambo ya kuchuja maji Nyankanga na kituo cha maji Nyankumbu , Mradi huo utasaidia zaidi ya watu 4000 kupata maji safi na salama. Pia, alitembelea mradi wa ushonaji wa akina mama na vijana wa kikundi cha Nyakatoma ambao unalenga kuwaendeleza vijana na wanawake ili kujipatia maendeleo. Vilevile alizindua mitambo ya ujenzi wa barabara yenye thamani ya tshs 2.1 bilioni fedha ambazo zilitokana na mapato ya ndani ya Halmashauri ya Mji Geita. Mitambo hiyo itasaidia kuboresha miundombinu ya barabara na kusidia kupunguza gharama katika mitambo ya kukodi na kuongeza kipato kwa Halmashauri hiyo.