MAWASILIANO YA BLOG

KWA MAONI NA USHAURI WASILIANA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO KWA SIMU NAMBA 0764 143 977 AU E-MAIL: habarigeita@gmail.com

Tuesday 25 November 2014

KATIBU TAWALA MPYA MKOA WA GEITA AKABIDHIWA RASMI OFISI AWATAKA WATUMISHI KUONYESHA USHIRIKIANO KATIKA UTENDAJI KAZI


Katibu Tawala Mkoa wa Geita ndugu Charles Pallangyo wakwanza kulia walio simama akikabidhiwa rasmi nyaraka za Ofisi na aliyekuwa Katibu Tawala Mkoa wa Geita Severine Kahitwa ambaye amehamia Mkoa wa Kilimanjaro.
Aliyekuwa Katibu Tawala Mkoa wa Geita  Ndugu Severine Kahitwa akiweka saini katika nyaraka mbalimbali za serikali na kumkabidhi rasmi nyaraka hizo Katibu Tawala mpya wa Mkoa wa Geita Ndugu Charles Pallangyo.

Katibu Tawala Mpya Mkoa wa Geita Ndugu Charles Pallangyo akizungumza na watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Geita na Taasisi nyingine za Umma na mashirika ambao walihudhuria Sherehe za Makabidhiano ya Ofisi kati yake na aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa huu Ndugu Severine Kahitwa. Katika makabidhiano hayo ndugu Pallangyo aliwataka watumishi kuonyesha ushirikiano na kufanya kazi kwa bidii katika majukumu yao ya kila siku huku akiwaagiza wakuu wa idara zote kuhakikisha kuwa wanafanya vikao na watumishi kila mwezi na muhtasari wa vikao hivyo unawasilishwa kwake mapema iwezekanavyo.Aidha aliwaomba wadau wote wa maendeleo kutoa ushirikiano katika masuala ya maendeleo ya Mkoa huu pale watakapohitajika kufanya hivyo.

Aliyekuwa Katibu Tawala Mkoa Mkoa wa Geita ambaye sasa ni Katibu Tawala Mkoa wa Kilimanjaro Ndugu Severine Kahitwa akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita wakati wa sherehe za kukabidhi Ofisi kwa Katibu Tawala Mpya wa Mkoa wa Geita.Katika sherehe hiyo iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita Ndugu Kahitwa aliwashukuru watumishi kwa ushirikiano waliompa wakati wa utendaji kazi wake katika Mkoa wa Geita na aliwataka kuendeleza mema hayo kwa kufanya kazi kwa bidii na uhadilifu wa hali ya juu kwa lengo la kuleta maendeleo katika Mkoa  wa Geita.

Baadhi ya wageni waalikwa na watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita,Taasisi za Umma na Mashirika wakiwa katika ukumbi wa Mikutato Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita wakifuatilia kwa karibu shughuli ya Makabidhiano ya Ofisi baina ya Katibu Tawala wa Mkoa anayehama ndugu Severine Kahitwa (Katibu Tawala Mkoa wa Kilimanjaro) na Katibu Tawala Mpya wa Mkoa wa Geita Ndugu Charles Pallangyo.

Makatibu Tawala wa Mikoa ya Geita na Kilimanjaro wapili na watatu kwa waliokaa kutoka kulia wakiwa katika picha ya pamoja Wakuu wa Idara Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita wakati wa sherehe za makabidhiano ya Ofisi baina ya ndugu Severine Kahitwa ambaye alikuwa Katibu Tawala Mkoa wa Geita ambaye anahamia Mkoa wa Kilimanjaro na ndugu Charles Pallangyo ambaye ndiye Katibu Tawala Mpya wa Mkoa wa Geita.

Makatibu Tawala wa Mikoa ya Geita na Kilimanjaro wapili na watatu (waliokaa) kutoka kulia wakiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Idara ya Utawala na rasilimali watu Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. katika sherehe za makabidhiano ya Ofisi baina ya viongozi hao.Wakwanza kushoto waliokaa ni Mkuu wa Idara ya Utawala na rasilimali watu Bw: Samsoni Mashalla na wakwanza kulia ni Afisa Utumishi Mwandamizi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita Bw: Magange .H. Mwita.

Monday 24 November 2014

Makatibu Tawala wa Mikoa ya Geita na Kilimanjaro wapili na watatu  walio kaa kutoka kulia wakiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa idara ya Elimu ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita wakati wa sherehe fupi ya makabidhiano ya Ofisi baina ya viongozi hao.Wengine walio kaa wakwanza kushoto ni Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali watu ndugu Samson Mashalla na wakwanza kulia ni Katibu Tawala Msaidizi Idara ya Elimu Bi Ephrasia Buchuma.

Makatibu Tawala wa Mikoa ya Geita na Kilimanjaro wapili na watatu walio kaa kutoka kulia wakiwa katika Picha ya pamoja na viongozi na wawakilishi wa Taasisi za Umma na binafsi wakati wa sherehe fupi za makabidhiano ya Ofisi baina ya aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita ndugu Severine Kahitwa ambaye amehamia Mkoa wa Kilimanjaro na Ndugu Charles Pallangyo Katibu Tawala mpya wa Mkoa wa Geita.

Wednesday 12 November 2014

MKUTANO WA TISA WA WADAU WA SEKTA NDOGO YA PAMBA WAFANYIKA MKOANI GEITA

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Geita Amani Mwenegoha akihutubia katika Mkutano wa wadau wa Sekta ndogo ya Pamba Mkoa wa Geita.Katika Mkutano huo ambao Mhe Amani alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa  Geita Mhe.Fatma Mwassa aliwapongeza kwa dhati viongozi wa Bodi ya Pamba kwa kushirikiana ta Tanzania Gastby Trust kwa kuendelea kuwezesha utaratibu wa wadau wa Pamba kukutana kila baada ya miezi mitatu uamuzi ambao utawanufaisha wakulima na Wafanyabiashara wa zao la Pamba Mkoa wa Geita.Mkutano huo ulikusudia kujadili kwa kina mkakati wa utekelezaji wa kilimo mkataba katika msimu 2014/2015, Mkakati wa kila halmashauri katika kuongeza uzalishaji wa Pamba kutoka kilo 400 kufikia kilo 800 kwa ekari.

Katibu Tawala msaidizi Idara ya Uchumi na uzalishaji ndugu Emili Kasagala akiwaongoza wajumbe wa Mkutano katika agenda za Mkutano wa wadau wa Sekta ndogo ya Pamba Mkoa wa Geita.

Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Pamba kanda ya Ziwa ndugu kalidushi Buruma akichangia mada kuhusu kilimo cha mkataba cha Pamba wakati wa Mkutano wa tisa wa Sekta ndogo ya Pamba Mkoa wa Geita.

Mwakilishi wa Kampuni ya Tanzania Gast Trust (TGT) Dr. Sililima akichangia mada kuhusu kilimo cha Pamba cha Mkataba wakati wa Mkutano wa tisa wa wadau wa Sekta ndogo ya Pamba Mkoa wa Geita.

Mwakilishi wa Kampuni ya Quton ndugu Benedicto Massele akitoa ufafanuzi kuhusu Mbegu za Pamba za Quton (mbegu zisizo na manyoya) wakati wa Mkutano wa tisa wa Sekta ndogo ya Pamba Mkoa wa Geita.

Afisa Kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale ndugu Gudala Kija akitoa maelezo kuhusu kilimo cha Pamba wakati wa Mkutano wa wadau wa Sekta ndogo ya Pamba Mkoa wa Geita.

Mkulima wa zao la Pamba Wilaya ya Nyang'hwale ndugu Masoud Mtore akichangia mada wakati wa Mkutano  wa tisa wa wadau wa Sekta ndogo ya pamba Mkoa wa Geita.


Wadau wa Sekta ndogo ya Pamba Mkoa wa Geita wakiwa katika ukumbi wa Mkutano wakati wa mkutano wa tisa wa sekta hiyo hivi karibuni Mkoani Geita.


Wadau wa Sekta ndogo ya Pamba Mkoa wa Geita wakifuatilia kwa makini Mkutano wa tisa wa sekta hiyo uliofanyika hivi karibuni Mkoani Geita.