MAWASILIANO YA BLOG

KWA MAONI NA USHAURI WASILIANA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO KWA SIMU NAMBA 0764 143 977 AU E-MAIL: habarigeita@gmail.com

Friday 11 November 2016

Mzee Atanazy Enyasi Mwenyekiti wa kamati ya madawati Mkoa wa Geita akizungumza  na kuwaomba wananchi na wadau wengine wa maendeleo kujitokeza na kuchangia madawati wakati wa hafla fupi ya Mkoa wa Geita kupokea madawati 100 kutoka katika mfuko wa hifadhi ya Jamii wa PSPF Geita.

Wanafunzi wakiwa wamekalia sehemu ya madawati iliyochangwa na mfuko wa hifadhi ya jamii wa PSPF

Mheshimiwa Meja Jenerali (Mst) Ezekiel Kyunga Mkuu wa Mkoa wa Geita akiwa na wanafunzi wa Shule ya Msingi Geita walioshiriki katika hafla fupi ya kukabidhi madawati  100 iliyoandaliwa na PSPF Geita katika viwanja vya Halmashauri ya Mji Geita.