Mzee Atanazy Enyasi Mwenyekiti wa kamati ya madawati Mkoa wa Geita akizungumza na kuwaomba wananchi na wadau wengine wa maendeleo kujitokeza na kuchangia madawati wakati wa hafla fupi ya Mkoa wa Geita kupokea madawati 100 kutoka katika mfuko wa hifadhi ya Jamii wa PSPF Geita.
Wanafunzi wakiwa wamekalia sehemu ya madawati iliyochangwa na mfuko wa hifadhi ya jamii wa PSPF
Mheshimiwa Meja Jenerali (Mst) Ezekiel Kyunga Mkuu wa Mkoa wa Geita akiwa na wanafunzi wa Shule ya Msingi Geita walioshiriki katika hafla fupi ya kukabidhi madawati 100 iliyoandaliwa na PSPF Geita katika viwanja vya Halmashauri ya Mji Geita.