MAWASILIANO YA BLOG

KWA MAONI NA USHAURI WASILIANA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO KWA SIMU NAMBA 0764 143 977 AU E-MAIL: habarigeita@gmail.com

Tuesday 21 October 2014


Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Geita Magalula Saidi akiwahutubia wananchi wakati wa Uzinduzi Chanjo ya Surua - Rubella ambao ulifanyika katika kituo cha Afya Nyankumbu Halmashauri ya Mji wa Geita. Mhe Mkuu wa Mkoa alitumia nafasi hiyo kuwakumbusha wazazi na wanajamii kuwa Chanjo ni haki ya kila mtoto na ni jukumu la kila mzazi au mlezi kuhakikisha kuwa watoto wanapata chanjo na huduma nyingine muhimu za afya kama matone ya vitamini A na dawa za minyoo.Aidha alitoa angalizo kwa wananchi kuwa kuna kazi kubwa ya kuwaelimisha kuhusu kampeni ya chanjo ya Surua-Rubella ambayo inatolewa sanjali na huduma nyingine hivyo aliwataka wasaidiane na serikali kupeleka taarifa sahihi kwa wenzao ili kuepusha upotoshaji. ''Kila mmoja wetu anawajibu wa kuelimisha na kuhamasisha mwenzake ili tuweze kujitokeza kwa wingi wakati wa kampeni kwa kuwaleta watoto wote kupata chanjo kwa faida ya Afya zao ,Mkoa na Taifa''. Aliwataka wananchi kuwapeleka watoto katika vituo vya kutolea chanjo ili wakingwe dhidi ya magonjwa yanayozuilika kwa chanjo na kuboresha maisha na afya zao.