MAWASILIANO YA BLOG

KWA MAONI NA USHAURI WASILIANA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO KWA SIMU NAMBA 0764 143 977 AU E-MAIL: habarigeita@gmail.com

Friday 19 December 2014

Afisa Elimu Mkoa wa Geita Bi. Ephrasia Buchuma akitoa taarifa ya Elimu Mkoa wa Geita kwa wajumbe wa kamati ya Kutangaza matokeo na kutangaza uteuzi wa wanafunzi watakaojiunga kidato cha kwanza mwaka 2015 Mkoa wa Geita. Katika taarifa hiyo Afisa Elimu alieleza kuwa hali ya ufaulu katika Mkoa hairidhishi sana japo kiwango cha ufaulu kimeongezeka kwa asilimia 11%  kutoka 52% mwaka 2013 hadi 63%  mwaka 2014. Hata hivyo, Mkoa wa Geita haukufikia lengo lake la 71% katika Mwaka huu hivyo aliwataka wadau wa elimu katika Mkoa kuongeza nguvu na bidii ili kuhakikisha kuwa Mkoa unapiga hatua zaidi katika masuala ya Elimu na kuongeza kiwango cha ufaulu. Aidha, Bi. Buchuma alitaja sababu za kutofanya vizuri kuwa ni mazingira magumu ya kazi kwa walimu, usimamizi duni wa elimu ngazi za halmashauri pamoja na utoro wa walimu, wanafunzi na kutozingatiwa kwa ratiba ya masomo kwa siku katika shule.