Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita Selestine Gesimba akisisitiza jambo wakati wa hafla fupi ya kukabidhiwa madawati 100 iliyoandaliwa na PSPF Geita. Ndugu Gesimba amewashukuru wadau wote wanaondelea kutekeleza ahadi yao walio ahidi wakati wa harambee ili kukamilisha na kumaliza tatizo la madawati katika Mkoa wa Geita.
Mheshimiwa Ezekiel Kyunga Mkuu wa Mkoa wa Geita akikabidhi madawati 100 kwa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Madawati Mkoa wa Geita ndugu Atanazy Enyasi na Ernest Nyororo. Madawati hayo kutoka PSPF yamekabidhiwa kwa Halmashauri ya Mbogwe.