MAWASILIANO YA BLOG

KWA MAONI NA USHAURI WASILIANA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO KWA SIMU NAMBA 0764 143 977 AU E-MAIL: habarigeita@gmail.com

Friday 11 November 2016

PSPF MKOA WA GEITA WACHANGIA MADAWATI 100 YENYE THAMANI YA TSHS 7.5 MILIONI MKOANI GEITA

Edward Temu Kaimu Mkurugenzi wa PSPF Mkoa wa Geita  akikabidhi madawati 100 yenye thamani ya shilingi 7,500,000/= kwa Mheshimiwa Ezekiel Kyunga Mkuu wa Mkoa wa Geita katika hafla fupi iliyofanyika katika viwanja vya Halmashauri ya Mji Geita. Mkuu wa Mkoa amewashukuru PSPF kwa mchango wao huo wenye manufaa katika Sekta ya Elimu Mkoani Geita na ametumia fursa hiyo kuwaomba wananchi na wadau wote wa maendeleo kuendelea kuchangia madawati ili kuhakikisha kwamba wanafunzi wote katika Mkoa wa Geita wanakaa kwenye madawati wakati wa masomo yao katika shule zote za Msingi na Sekondari. Madawati yote yaliyopokelewa yamepelekwa Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe ili kupunguza uhaba huo katika Halmashauri hiyo. 

Mwenyekiti wa kamati ya Madawati Mkoa wa Geita Atanazy Enyasi akizungumza na ndugu  Elias Kayandabila Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe baada ya kumkabidhi madawati 100 yenye thamani ya shilingi 7.5 Milioni ikiwa ni mchango wa shirika la PSPF Mkoa wa Geita.

Viongozi mbalimbali wa Serikali Mkoa wa Geita wakiwa wamekaa pamoja na wanafunzi kwenye madawati 100 yaliyotolewa na PSPF Mkoa wa Geita.