WAKURUGENZI GEITA
WATAKIWA KUWEKA UTARATIBU MZURI KWA VIKUNDI KWENDA KUJIFUNZA UFUGAJI NYUKI
WILAYA YA BUKOMBE:
Wakurugenzi wa Halmashauri za wilaya Mkoani Geita wametakiwa
kuweka utaratibu mzuri wa vikundi vya wafuga nyuki kwenda kujifunza namna bora
ya ufugaji nyuki katika wilaya ya Bukombe ambayo imefanikiwa kwa kiasi kikubwa
katika zao la nyuki.