MAWASILIANO YA BLOG

KWA MAONI NA USHAURI WASILIANA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO KWA SIMU NAMBA 0764 143 977 AU E-MAIL: habarigeita@gmail.com

Wednesday 19 August 2015

MWENGE WA UHURU 2015 WAZINDUA, KUFUNGUA NA KUWEKA MAWE YA MSINGI KATIKA MIRADI YA MAENDELEO 67 YENYE THAMANI YA TSHS. BILIONI 4,464,623,474/= MKOANI GEITA.

Askari na wananchi wa Mkoa wa Geita kwa pamoja wakiukimbiza Mwenge wa Uhuru ulipokuwa Mkoani Geita kuanzia tarehe 10/08/2015 hadi tarehe 16/08/2015. Mwenge ulikimbizwa katika Wilaya zote 5 za Mkoa wa Geita na katika Halmashauri za Wilaya 6 kwa umbali wa Kilometa 664.13 katika miradi 67 ya maendeleo yenye thamani ya Tshs. Bilioni 4,464,623,474/=.

Mheshimiwa Fatma Mwassa Mkuu wa Mkoa Geita akikabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Nassoro Rufunga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga tarehe 16/08/2015 baada ya kutembelea, kukagua, kuzindua na kuweka mawe ya msingi katika jumla ya miradi ya maendeleo 67 ya Mkoa wa Geita. Miradi hiyo inathamani ya Tshs Bilioni 4,464,623,471/= fedha ambazo ni michango ya serikali kuu, wananchi, Halmashauri za Wilaya na Wahisani mbalimbali.

Mradi wa Tanki la maji Kilimahewa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe ambao ulizinduliwa na Mbio za Mwenge wa Uhuru 2015 unaosaidia zaidi ya wananchi 2500 wa Ushirombo.

Mradi wa kisima kirefu cha Maji katika Kijiji cha Nyamalulu Halmashauri ya Wilaya Geita. Mradi huu ulizinduliwa na mbio za Mwenge 2015 hivyo kuwafanya wananchi wa kijiji hicho kupata maji safi na salama.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa 2015 Juma Chum akizindua Trekta la Kijiji cha Nyamalulu Halmashauri ya Geita wakati wa mbio hizo wilayani Geita.Mradi huu unatarajia kusaidia wananchi katika usafirishaji wa mbolea mashambani na pia katika shughuli za kilimo kama vile kulima  maeneo makubwa hivyo kuongeza uzalishaji wa mazao.


Baadhi ya wananchi na watumishi waserikali wakigusa Mwenge wa Uhuru ulipokuwa Mkoani Geita tarehe 10-16/08/2015.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge akimkabidhi mama Chandarua chenye dawa kuonyesha juhudi za serikali  za kupambana na ugonjwa wa malaria ili kuhakikisha kuwa wananchi wanakuwa na afya njema wakati wote.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge 2015 Juma Chum akikabidhi mzinga wa nyuki kwa kikundi cha wajasiliamali wanawake cha Ufugaji Nyuki wakati wa Mbio za Mwenge Mkoani Geita.Hii ni kuonyesha namna serikali inavyowasaidia wanawake ili waondokane na umaskini kwa kuwaunganisha katika vikundi ili wazalishe na kujipatia kipato.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa 2015 ndugu Juma Chum akizindua mradi wa maji bomba katika kijiji cha Kikumbaitare Halmashauri ya Wilaya Chato. Mradi huu utanufaisha watu zaidi ya 1500 ambao walikuwa wakitembea umbali mrefu kutafuta maji.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge 2015 ndugu Juma Khatibu Chum akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Geita Fatma Mwassa baada ya kuwasili Mkoa wa Geita, wengine katika mstari ni kamati ya ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Geita.

Mheshimiwa Fatma Mwassa Mkuu wa Mkoa wa Geita akikabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Chato manzie Mangochie baada ya Mwenge kuwasili Mkoani Geita ukitokea Mkoa wa Kagera na kupokewa katika kijiji cha Mkolani Wilaya ya Chato.

Mheshimiwa Fatma Mwassa Mkuu wa Mkoa wa Geita (aliye vaa suti nyeusi) akikabidhiwa Mwenge wa Uhuru na Mheshimiwa John Mongella Mkuu wa Mkoa wa Kagera katika kijiji cha Mkolani Halmashauri ya Chato baada ya Mwenge kuwasili Mkoa wa Geita.

Msanii wa kikundi cha sanaa cha ngoma za asili akitumbuiza wakati wa mapokezi ya Mwenge wa Uhuru Mkoani Geita tarehe 10/08/2015.

Friday 10 July 2015

FAHAMU YALIYOJILI MKOANI GEITA WAKATI WA UFUNGUZI WA TAMASHA LA LIVE YOUR GOALS NA MAFUNZO YA GRASSROOTS YALIYOANDALIWA NA TFF PAMOJA NA FIFA

Mheshimiwa Fatma Mwassa Mkuu wa Mkoa Geita akizumgumza na wadau wa mpira wa miguu wa wanawake pamoja na wananchi (hawapo katika picha) wakati wa ufunguzi wa Tamasha la  LIVE YOUR GOALS na Mafunzo ya Grassroots kwa walimu wa shule za msingi yaliyofanyika katika Mkoa wa Geita kwa lengo la kuhamasisha watoto wa kike kushiriki katika mpira wa miguu.  Katika Tamasha hilo mheshimiwa Fatma Mwassa alitoa rai kwa wazazi wote kuona umuhimu wa kuwaruhusu watoto wao wa kike kushiriki katika michezo hususani mpira wa miguu kwakua michezo ni fursa na inasaidia kujenga mwili na akili na pia kuna fursa nyingi za kimaendeleo.  Pia aliwapongeza walimu wote waliopata mafunzo hayo na kuwataka kutumia ujuzi huo kwa faida ya mkoa wa Geita na Taifa kwa ujumla. "Nafahamu kuwa walimu kutoka wilaya zote na Halmashauri sita za Mkoa wa Geita wameshiriki ipasavyo katika mafunzo haya, ni imani yangu taaluma hii itafika katika shule zote za Mkoa wa Geita ili kufanya program hii kuwa endelevu''.  Hata hivyo aliwapongeza FIFA na TFF kwa kuuchagua Mkoa wa Geita kuwa wakwanza katika kutekeleza program hii ambapo aliahidi kuanzisha mashindano mengine katika Mkoa yatakayojulikana kwa jina la Blatter Cup (IF YOU DO FIFA DOES)

Ndugu Henry Tandau Mkurugenzi wa ufundi na utawala wa shirikisho la mpira wa miguu duniani (FIFA) akimkabidhi mgeni rasmi Bi: Fatma Mwassa zawadi ya mipira wakati wa ufunguzi wa Tamasha la LIVE YOUR GOALS lililofanyika shule ya Sekondari Nyankumbu Mkoani Geita.

Mheshimiwa Fatma Mwassa Mkuu wa Mkoa wa Geita akikabidhi zawadi ya mipira kwa mmoja wa washiriki baada ya kufanya vizuri katika Tamasha, kushoto ni Mheshimiwa  Manzie Mangochie Mkuu wa wilaya ya Geita.

Mwenyekiti wa kamati ya maendeleo ya mpira wa wanawake kutoka TFF Ndugu Kiondo akizungumza na wadau wa mchezo wa mpira wa miguu Mkoani Geita wakati wa ufunguzi wa Tamasha la LIVE YOUR GOALS.

Thursday 9 July 2015

Mwenyekiti wa chama cha mpira wa miguu Geita (GEREFA) Salum Kulunge akizungumza kuhusu maendeleo ya mpira wa miguu ndani ya Mkoa wa Geita wakati wa ufunguzi wa Tamasha la LIVE YOUR GOALS na Mafunzo ya Grassroots Mkoani Geita.

Mheshimiwa Fatma Mwassa Mkuu wa Mkoa wa Geita akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa chama cha mpira wa miguu Geita (GEREFA) na mabalozi wa mchezo wa mpira wa wanawake nchini. Wanne kutoka kushoto ni Mheshimiwa Manzie Mangochie Mkuu wa Wilaya ya Geita.

Mheshimiwa Fatma A. Mwassa Mkuu wa Mkoa wa Geita ( mstari wa kwanza aliyevaa Tshirt nyeupe katikati ya watoto) akiwa katika picha ya pamoja na watoto wakike walioshiriki katika tamasha la LIVE YOUR GOALS Mkoani Geita.

Baadhi ya watoto wakike wakicheza mpira wa miguu katika viwanja vya shule ya sekondari ya wasichana Nyankumbu wakati wa ufunguzi wa Tamasha la LIVE YOUR GOALS na mafunzo ya Grassroots Mkoani Geita. Mafunzo hayo yaliandaliwa na TFF pamoja na FIFA.

Monday 6 July 2015


Baadhi ya washiriki wa Tamasha la LIVE YOUR GOALS kutoka Wilaya mbalimbali za Mkoa wa Geita wakiwasili katika viwanja vya michezo Nyankumbu Mkoani Geita.

Baadhi ya wanamichezo na wadau mbalimbali wa michezo waliojitokeza kushuhudia Ufunguzi wa Tamasha la LIVE YOUR GOAL na Mafunzo ya Grass Roots kwa Mpira wa wanawake uliofanyika  katika  uwanja wa michezo wa shule ya sekondari Nyankumbu Wilaya ya Geita.

Thursday 30 April 2015

FAHAMU YALIYOJILI KATIKA KIKAO CHA BARAZA LA WAFANYAKAZI MKOA WA GEITA LILILOFANYIKA TAREHE 29/04/2015

Mwenyekiti wa Baraza la wafanyakazi Mkoa wa Geita Ndugu Charles Pallangyo (katikati kwa waliokaa meza ya mbele) akiwahutubia wajumbe wa baraza hilo wakati wa kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa Geita ambapo aliwataka wajumbe hao kuhakikisha kuwa wanaelimisha wafanyakazi wengine katika maeneo yao kufanya kazi kwa kuzingatia sheria na kanuni za Utumishi wa Umma katika utoaji wa huduma kwa wananchi. Aidha Ndugu Charles Pallangyo ambaye pia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita aliwataka wafanyakazi wote wa Mkoa wa Geita kufanya kazi kwa kuzingatia utawala bora na kujiepusha na vitendo vyote vinavyoashiria rushwa na kutimiza wajibu ili wananchi waendelee kuiamini serikali. Vilevile aligusia suala la UKIMWI katika mazingira ya kazi ambapo aliwataka wafanyakazi wote kujilinda na kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huo hatari ambapo aliwataka kuhakikisha wanajenga tabia ya kupima afya mara kwa mara na wale wanaokutwa na maambukizi wajitokeze wapate huduma kwasababu serikali inawahudumia watumishi wa namna hiyo kwa kuwapatia fedha ya matibabu pamoja na lishe na kwa wale ambao hawana maambukizi walitakiwa kujilinda na kijiepusha na vitendo vinavyoweza kusababisha wao kuambukizwa ugonjwa huo hatari kwa taifa na dunia.Aidha aliwataka wajumbe na wafanyakazi kuwa wavumilivu kwakuwa serikali inatambua kero zao na inazitafutia ufumbuzi kwa lengo la kuboresha maisha yao.

Katibu wa Chama cha wafanyakazi (TUGHE) Mkoa wa Geita  Bi. Ethel Kahuluda akizungumza na wajumbe wa baraza ambapo aliwaeleza namna wafanyakazi wanavyotakiwa kuwa wakati wa kutimiza majukumu yao ya kila siku na pia pale wanapozungumza na viongozi au waajiri wao. Alisema kuwa wafanyakazi wana kero nyingi zinazowakabili lakini ni vyema wakawa wavumilivu na watulivu wakati wa kudai haki zao za msingi napia wahakikishe kuwa pamoja na kudai haki hizo pia watimize wajibu wao ipasavyo wakati wa kuhudumia wananchi.

Katibu wa Baraza la wafanyakazi Mkoa wa Geita Bi. Sania Mwangakala akiwakaribisha wajumbe wa baraza hilo pamoja na Mwenyekiti wa Baraza Ndugu Charles Pallangyo ambaye pia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita(katikati) pamoja na Katibu wa Chama cha wafanyakazi Mkoa wa Geita(TUGHE) Bi. Ethel Kahuluda wa kwanza kulia. Katika kikao hicho Bi. Sania aliwaeleza wajumbe kuwa madhumuni ya kikao hicho ni kujadili changamoto zinazowakabili wafanya kazi na kuzitafutia ufumbuzi.Hata hivyo katika kikao hicho kulifanyika uchaguzi wa katibu wa baraza hilo baada ya Bi. Sania kuwa na majukumu mengine ya kikazi hivyo nafasi yake kuchukuliwa na ndugu Magange Hamisi Mwita na naibu katibu kuwa ndugu Sara Mwangole wote kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita.

Mratibu wa UKIMWI Mkoa wa Geita Dkt. Joseph Odero akiwasilisha mada kuhusu UKIMWI ambapo aliwataka wajumbe kuwahamasisha wafanyakazi kuwa na tabia ya kupima virus vya UKIMWI na pale watakapo jitambua kuwa wameathirika wajitokeze ili wapate huduma, pia kama hawajaambukizwa ni bora wakatumia njia za kujikinga na maradhi hayo au kuwa waaminifu au kujizuia kabisa.

Mjumbe wa baraza la wafanyakazi Mkoa wa Geita ndugu D.B Kayango ambaye pia ni Katibu Tawala Msaidizi Idara ya Mipango Mkoa wa Geita akiwasilisha bajeti ya Mkoa wa Geita kwa Mwaka 2015/2016 mbele ya wajumbe wa kikao cha baraza hilo kilichofanyika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Mjumbe wa baraza la wafanyakazi la Mkoa wa Geita Ndugu Mathayo Maselle akichangia Mada kuhusu UKIMWI iliyowasilishwa na Mratibu wa UKIMWI Mkoa Dkt. Joseph Odero wakati wa kikao.

Mganga Mkuu wa Mkoa Geita Dkt. Joseph Kisala akitoa ufafanuzi  kwa wajumbe wa baraza la wafanyakazi Mkoa wa Geita wakati wa kikao kilichofanyika tarehe 29/04/2015 kuhusu utaratibu wa malipo ya posho ya muda wa ziada wa kazi kwa madaktari na wauguzi wa hospitali, Vituo vya Afya na Zahanati.

Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi Mkoa wa Geita wakifuatilia kwa karibu makaburasha wakati  wa kikao cha baraza hilo kilichofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Geita kwa lengo la kujadili changamoto zinazowakabili wafanyakazi na kuzitafutia ufumbuzi.(Picha-Afisa Habari RS-GEITA)

Thursday 26 March 2015

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI ATEMBELEA MKOA WA GEITA WANANCHI WATAKIWA KUSHIRIKIANA NA WAWEKEZAJI ILI KUJILETEA MAENDELEO NA KUKUZA UCHUMI WA NCHI.

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya uchimbaji madini ya Geita Gold Mine (GGML) Michael Van Anen akimkabidhi waziri wa Nishati na Madini hundi ya  tshs bilioni 2.23 kama ushuru wa tozo (service levy) kwa halmashauri  ya Geita na halmashauri ya Geita mjini wakati wa hafla hiyo iliyofanyika katika viwanja vya Halmashauri ya mji wa Geita na kuhudhuriwa na viongozi wa taasisi mbalimbali za serikali ,dini na binafsi.

Mhe. George Simbachawene Waziri wa Nishati na Madini akiwakabidhi hundi ya Tshs bilioni 2.23 wenyeviti wa Halmashauri ya Geita na Halmashauri ya Geita Mjini. Fedha hiyo inatokana na kodi ya ushuru wa tozo (service levy) iliyolipwa na kampuni ya uchimbaji wa madini ya Geita (GGML). Aliwataka Wenyeviti hao kuhakikisha kuwa fedha hizo zinafanya kazi za maendeleo na siyo vinginevyo ili kukuza uchumi na maendeleo ya Mkoa wa Geita. Hata hivyo aliwaeleza wananchi kuwa watarajie kuona huduma bora zaidi kwenye elimu, afya, barabara, umeme na maji. Kampuni ya GGM imekuwa ikisaidia katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Mkoa huu kama vile ujenzi wa shule,ujenzi wa nyumba za watumishi na kituo cha afya Nyakabale, maji na kituo cha ushauri nasaha Geita.

Mhe.Fatma Mwassa Mkuu wa Mkoa wa Geita akizungumza na wananchi wa Mji wa Geita wakati wa Ziara ya Waziri wa  Nishati na Madini Mkoa Geita hivi karibuni.


Mhe. George Simbachawne Waziri wa Nishati na Madini akikagua shughuli za uchimbaji wa madini ya dhahabu katika Mdodi wa Busolwa Mine wakati wa Ziara yake Mkoa wa Geita.
Mwekezaji wa ndani ambaye pia ni mmiliki wa kampuni ya uchimbaji wa madini ya Busolwa Mine Baraka Ezekiel akimwelezea waziri namna shughuli za uchimbaji wa madini zinavyofanyika katika Mgodi huo wakati wa ziara ya Waziri wa Nishati na Madini Mkoa wa Geita. Kushoto kwa Mhe. Waziri ni mhe Fatma Mwassa Mkuu wa Mkoa wa Geita na Mhe.Agustino Maselle Mbunge wa Jimbo la Mbogwe Mkoa wa Geita.
Mhe. George Simbachawene Waziri wa Nishati na Madini akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa mgodi wa Busolwa Mine alipotembelea Mgodi huo Nyarugusu Mkoani Geita. Mstari wa Mbele waliokaa kutoka kilia  kwa Waziri wapili ni Agustino Maselle Mbunge wa Mbogwe, ndugu Charles Pallangyo Katibu Tawala Mkoa wa Geita na kushoto kwa waziri ni ndugu Baraka Ezekiel Meneja wa Busolwa Mine,Mhe.Fatma Mwassa Mkuu wa Mkoa Geita na Mhe. Manzie Mangochie Mkuu wa Wilaya ya Geita.

Mhe. Fatma Mwassa Mkuu wa Mkoa wa Geita akiongozana na Mhe. George Simbachawene  Waziri wa Nishati na Madini wakati wa ukaguzi wa miundombinu ya maji ambayo inatarajia kusambaza maji mjini Geita. Mradi huo wa maji wa Mjini Geita unatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na Kampuni ya uchimbaji wa madini Geita (GGML). Mradi huo unatarajiwa kukamilika mapema mei 2015.

Mhe. George Simbachawene Waziri wa Nishati na Madini akikata utepe kuashilia kufungua nyumba 18 za wananchi wa Buhalahala ambazo zimejengwa na Mgodi wa Geita kama fidia baada ya kuchukua maeneo ya wananchi hao.Wapili kulia kwa Waziri ni Mhe. Fatma Mwassa Mkuu wa Mkoa wa Geita na kushoto ni Meneja wa Mgodi wa Geita Bw. Michael Van Anen.


Mhe.Waziri wa Nishati na Madini akizungumza na wananchi wa buhalahala baada ya kuweka jiwe la msingi la uzinduzi kwenye nyumba 18 za wananchi hao.

Moja ya nyumba 18 ambazo zimewekwa jiwe la msingi la uzinduzi na Mhe. George Simbachawene Waziri wa Nishati na Madini wakati wa ziara yake Mkoa wa Geita.Nyumba hii ina vyumba vitatu vya kulala ,sitting room, jiko na stoo.

Mhe.George Simbachawene Waziri wa Nishati na Madini akiwa katika picha ya pamoja na wananchi wa buhulahala wilaya ya Geita baada ya kuweka jiwe la msingi la uzinduzi wa nyumba 18 za wananchi hao ambazo ni fidia kwao kutoka Mgodi wa Dhahabu wa Geita baada ya kuhamishwa kutoka katika maeneo yao kupisha shughuli za uchimbaji madini.Viongozi wengine waliohudhuria katika tukio hilo ni Mhe. Fatma Mwassa Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Manzie Mangochie Mkuu wa Wilaya ya Geita na Meneja wa mgodi wa Geita ndugu Michael Van Anen.


Wananchi wa Mkoa wa Geita hususani mjini Geita wakiwa wamejitokeza kwa wingi kumsikiliza Mhe. George Simbachawene Waziri wa Nishati na Madini (hayupo pichani) wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku mbili Mkoa wa Geita.


Wednesday 11 March 2015

MKOA WA GEITA WAWAFARIJI WAANGA WA MAAFA YA MVUA KUBWA HUKO MWAKATA WILAYA YA KAHAMA



Mhe. Fatma Mwassa Mkuu wa Mkoa wa Geita akimkabidhi Benson Mpesya Mkuu wa Wilaya ya Kahama Gunia la mchele kuwakilisha bidhaa nyingine zilizotolewa na Mkoa wa Geita kwa wananchi wa kijiji cha Mwakata ambao walipatwa na maafa yaliyosababishwa na mvua kubwa na upepo mkali na kupelekea watu zaidi ya 30 kupoteza maisha pamoja na uharibifu mkubwa wa mali za wananchi ikiwemo mifugo na makazi.Katika salamu zake Mkuu wa Mkoa alitoa rai kuwa msaada huo utumike kama ulivyokusudiwa na kuwafike walengwa.Aidha, aliwataka wananchi kuwa watulivu wakati serikali na wadau wengine wakiendelea na jitihada za kuwasaidia.Bidhaa zilizotolewa na Mkoa wa Geita ni pamoja na Mchele, Maharage, Unga n.k.Mkuu wa Mkoa aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa Bw. Charles Pallangyo pamoja na wakurugenzi wote wa Halmashauri za Mkoa wa Geita.