MAWASILIANO YA BLOG

KWA MAONI NA USHAURI WASILIANA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO KWA SIMU NAMBA 0764 143 977 AU E-MAIL: habarigeita@gmail.com

Sunday 24 April 2016

MKUU WA MKOA WA GEITA MEJA JENERALI EZEKIEL KYUNGA ATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA NYUMBA 18 ZA WATUMISHI, HOSPITALI TEULE YA MKOA WA GEITA NA SOKO LA WAKULIMA NYANKUMBU HALMASHAURI YA MJI GEITA


Mheshimiwa Ezekiel Kyunga Mkuu wa Mkoa Geita akizungumza na mjasiliamali wa kuuza viazi vitamu Bi. Aneth Mabula katika Soko la wakulima Nyankumbu Halmashauri ya Mji Geita alipotembelea soko hilo hivi karibuni. Akiwa sokoni hapo Mkuu wa Mkoa alisisitiza suala la usafi katika maeneo yote ya Soko. Aidha aliwaeleza wafanya biashara kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha ina boresha soko hili ili wananchi wafanye biashara katika mazingira mazuri na salama kwa afya za wateja wao.


Katika ziara hiyo Mkuu wa pia alipata fursa ya kutembelea Hospitali Teule ya Mkoa wa Geita kwa lengo la kuona namna huduma kwa wananchi zinavyotolewa katika Hospitali hiyo. Aidha, alipongeza juhudi za kampuni ya Mgodi wa Geita (GGML) Katika kusaidia kuboresha huduma za afya kwa kununua vifaa vya kisasa.  Hata hivyo aliwataka watumishi wa Idara hiyo kufanya kazi kwa weledi ili kutatua matatizo ya wananchi wanaofika katika Hospitali hiyo kupata Huduma.

Moja ya Nyumba za watumishi wa Halmashauri ya Mji Geita zilizotembelewa na Mkuu wa Mkoa wa Geita katika eneo la Bombambili.Nyumba hizi zimejengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC)

Mkuu wa Mkoa  wa Geita akiongozana na viongozi  wa Wilaya ya Geita kukagua mradi wa nyumba 18 za watumishi  zilizonunuliwa na Halmashauri ya Mji Geita kutoka Shirirkr la nyumba la taifa (NHC) ili kusaidia kuboresha makazi ya watumishi katika Halmashauri hiyo.(Wakwanza kulia ni Manzie Mangochie Mkuu wa Wilaya ya Geita).


Baadhi ya nyumba zilizotembelewa na kukaguliwa zinavyoonekana.Nyumba hizi zina uwezo wa kuhudumia familia mbili kwa wakati mmoja.

Watumishi pamoja na viongozi wa Serikali Mkoani Geita wakifuatilia kwa karibu maelekezo ya  Mkuu wa Mkoa wa Geita alipofanya ziara katika Halmashauri ya Mji Geita.

Mheshimiwa Meja Jenerali (Mstaafu) Ezekiel Kyunga Mkuu wa Mkoa wa Geita akizungumza na vyombo vya Habari pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali Mkoani Geita kueleza madhumuni ya Ziara yake katika Halmashauri ya Mji Geita.

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Mji Geita Ndugu Max Kamaoni akisoma taarifa ya miradi ya maendeleo ambayo imetembelewa na Mheshimiwa  Meja Jenerali (Mstaafu) Ezekiel Kyunga Mkuu wa Mkoa wa Geita (hayupo kwenye picha) wakati wa ziara yake ya kikazi katika Halmashauri hiyo tarehe 23/04/2016.(PICHA  OFISI YA RC - GEITA).