MAWASILIANO YA BLOG

KWA MAONI NA USHAURI WASILIANA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO KWA SIMU NAMBA 0764 143 977 AU E-MAIL: habarigeita@gmail.com

Friday 6 June 2014

'' NI MARUFUKU KUKOPA PAMBA KUTOKA KWA WAKULIMA''

Mwenyekiti wa kikao cha wadau wa Sekta ndogo ya Pamba Mkoa wa Geita Mhe. Magalula Saidi ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Geita akihutubia katika kikao cha sita cha sekta hiyo kilichofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Geita.Kaika kikao hicho Mhe.Mkuu wa Mkoa aliyataka makampuni yote yanayonunua pamba ndani ya Mkoa wa Geita kutokopa Pamba kutoka kwa Wakulima.


Mkoa wa Geita umepiga marufuku kwa makampuni ya uchambuzi na ununuzi wa pamba kuacha tabia ya kukopa pamba kutoka kwa wakulima.

Akizungumza katika kikao cha sita cha wadau wa sekta ndogo ya pamba Mkoa wa Geita Mwenyekiti wa kikao hicho Magalula Saidi ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Geita alisema kuwa ‘’ ni marufuku kwa kampuni yeyote ile inayonunua pamba katika Mkoa wa Geita kukopa pamba kutoka kwa wakulima kwani kufanya hivyo ni kumdumaza mkulima na kumcheleweshea maendeleo yake ya kila siku’’.

Mkoa wa Geita unatekeleza kilimo cha pamba cha mkataba ambapo wakulima wanakopeshwa pembejeo  bora kutoka kwa makampuni ili wazalishe kwa wingi na wanufaike na kilimo hicho.


Kikao cha sita cha wadau wa sekta ndogo ya pamba Mkoa wa Geita kilifanyika kwa lengo la kufanya tathimini ya kilimo hicho na changamoto zake kwa msimu unaokwisha 2013/2014 na pia kujadili namna  kilimo hicho kitakavyoendeshwa kwa msimu ujao.Hatahivyo wakulima wengi wa Mkoa wa Geita wanaonyesha kukubaliana na kilimo hicho ambacho inasemekana kina tija kwao.