MAWASILIANO YA BLOG

KWA MAONI NA USHAURI WASILIANA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO KWA SIMU NAMBA 0764 143 977 AU E-MAIL: habarigeita@gmail.com

Thursday 30 April 2015

FAHAMU YALIYOJILI KATIKA KIKAO CHA BARAZA LA WAFANYAKAZI MKOA WA GEITA LILILOFANYIKA TAREHE 29/04/2015

Mwenyekiti wa Baraza la wafanyakazi Mkoa wa Geita Ndugu Charles Pallangyo (katikati kwa waliokaa meza ya mbele) akiwahutubia wajumbe wa baraza hilo wakati wa kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa Geita ambapo aliwataka wajumbe hao kuhakikisha kuwa wanaelimisha wafanyakazi wengine katika maeneo yao kufanya kazi kwa kuzingatia sheria na kanuni za Utumishi wa Umma katika utoaji wa huduma kwa wananchi. Aidha Ndugu Charles Pallangyo ambaye pia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita aliwataka wafanyakazi wote wa Mkoa wa Geita kufanya kazi kwa kuzingatia utawala bora na kujiepusha na vitendo vyote vinavyoashiria rushwa na kutimiza wajibu ili wananchi waendelee kuiamini serikali. Vilevile aligusia suala la UKIMWI katika mazingira ya kazi ambapo aliwataka wafanyakazi wote kujilinda na kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huo hatari ambapo aliwataka kuhakikisha wanajenga tabia ya kupima afya mara kwa mara na wale wanaokutwa na maambukizi wajitokeze wapate huduma kwasababu serikali inawahudumia watumishi wa namna hiyo kwa kuwapatia fedha ya matibabu pamoja na lishe na kwa wale ambao hawana maambukizi walitakiwa kujilinda na kijiepusha na vitendo vinavyoweza kusababisha wao kuambukizwa ugonjwa huo hatari kwa taifa na dunia.Aidha aliwataka wajumbe na wafanyakazi kuwa wavumilivu kwakuwa serikali inatambua kero zao na inazitafutia ufumbuzi kwa lengo la kuboresha maisha yao.