MAWASILIANO YA BLOG

KWA MAONI NA USHAURI WASILIANA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO KWA SIMU NAMBA 0764 143 977 AU E-MAIL: habarigeita@gmail.com

Thursday 30 April 2015

Katibu wa Baraza la wafanyakazi Mkoa wa Geita Bi. Sania Mwangakala akiwakaribisha wajumbe wa baraza hilo pamoja na Mwenyekiti wa Baraza Ndugu Charles Pallangyo ambaye pia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita(katikati) pamoja na Katibu wa Chama cha wafanyakazi Mkoa wa Geita(TUGHE) Bi. Ethel Kahuluda wa kwanza kulia. Katika kikao hicho Bi. Sania aliwaeleza wajumbe kuwa madhumuni ya kikao hicho ni kujadili changamoto zinazowakabili wafanya kazi na kuzitafutia ufumbuzi.Hata hivyo katika kikao hicho kulifanyika uchaguzi wa katibu wa baraza hilo baada ya Bi. Sania kuwa na majukumu mengine ya kikazi hivyo nafasi yake kuchukuliwa na ndugu Magange Hamisi Mwita na naibu katibu kuwa ndugu Sara Mwangole wote kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita.