MAWASILIANO YA BLOG

KWA MAONI NA USHAURI WASILIANA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO KWA SIMU NAMBA 0764 143 977 AU E-MAIL: habarigeita@gmail.com

Friday 15 November 2013

RAIS KIKWETE AZINDUA RASMI MKOA WA GEITA.




Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe.Jakaya Mrisho Kikwete amewataka  viongozi na wazazi  Mkoa wa Geita kuhakikisha kuwa wanafunzi  wote walioacha masomo kwasababu mbalimbali wanatafutwa na kurudishwa shuleni.

Katika hotuba yake ya kuzindua Mkoa wa Geita na mpango mkakati wa Mkoa katika uwanja wa michezo wa Kalangalala Rais Kikwete amesema kuwa idadi ya wanafunzi wanaoandikishwa kuanza shule ni kubwa kuliko wanafunzi wanaohitimu masomo katika mkoa wa Geita hivyo ni lazima serikali serikali ifanye jitihada kubwa.

 

Mhe Rais anasema ‘’Viongozi  wa Mkoa na Halmashauri hakikisheni watoto wote walioacha masomo wanatafutwa popote walipo kwa kuunda sheria ndogondogo zinazowabana wazazi ili watoe msukumo  kwa watoto wao kwenda shule tusipofanya hivyo tutakuwa na Mkoa wenye wananchi wengi wasiojua kusoma na kuandika na hivyo kuchelewesha maendeleo’’.

 

Aidha katika mkutano huo Mhe. Rais amekabidhiwa hundi ya shiringi 25 millioni kutoka Benki ya NMB ikiwa ni sehemu ya mchango wa kusaidia huduma za afya katika mkoa wa Geita.

 

Katika ziara hiyo ya siku tano ndani ya Mkoa wa Geita Rais Kikwete anatarajia kuweka mawe ya msingi katika miradi mitatu  ya maendeleo inayotekelezwa na serikali ukiwemo ujenzi wa barabara mbili kwa kiwango cha lami za Bwanga-Biharamulo urefu 67 KM na Bwanga-Uyovu  urefu 45 KM,na ofisi ya CCM Chato,  Kufanya mikutano ya hadhara saba katika maeneo mbalimbali,  kufungua miradi miwili ya maendeleo ya Ng’anzo shule ya msingi na zahanati ya Kasota.

 

Pia Mhe.Rais Kikwete atazindua miradi mitano ya maendeleo ikiwemo mradi mmoja (1) wa maji katika kijiji cha Nyakafuru,  kuzindua miradi miwili ya uchenjuaji wa dhahabu katika maeneo ya Nyamigogo na Katente katika wilaya za Nyang’hwale na Mbogwe, kuzindua mradi wa umeme huko Katoro –Geita na Wodi ya akina mama.

 

Aidha Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atatembelea na kukagua miradi miwili ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa Theatre katika kituo cha afya Iboya na Mgodi mdogo wa Baraka Gold Mine huko Nyaruyeye wilaya ya Geita.