MAWASILIANO YA BLOG

KWA MAONI NA USHAURI WASILIANA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO KWA SIMU NAMBA 0764 143 977 AU E-MAIL: habarigeita@gmail.com

Monday 14 July 2014

Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Geita Magalula Saidi akikata utepe katika pikipiki 20 na Baiskeli 4 zilizotolewa na Kikundi cha wafanya biashara katika Mji wa Geita kwa lengo la kurahisisha kazi ya Askari Polisi katika kupambana na vitendo vya uharifu hasa katika maeneo yasiyopitika.Msaada huo kutoka kwa wafanya biashara umekuja baada ya Askari Polisi kwa kushirikiana na wananchi kufanikiwa kuwakamata majambazi wanaohusika na unyanganyi wa kutumia silaha.katika hafla hiyo Mkuu wa Mkoa aliwataka wananchi wote Mkoa wa Geita kuhakikisha kuwa wanatoa taarifa kwa jeshi la polisi kuhusu vitendo vinavyohusu uvunjifu wa amani.