MAWASILIANO YA BLOG

KWA MAONI NA USHAURI WASILIANA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO KWA SIMU NAMBA 0764 143 977 AU E-MAIL: habarigeita@gmail.com

Monday 14 July 2014

WILAYA YA BUKOMBE YATOA MAFUNZO YA WALIMU KATIKA KATA ZOTE

Afisa Elimu Mkoa wa Geita Ephrasia Buchuma akifunga mafunzo ya Walimu wa Wilaya ya Bukombe.Jumla ya Walimu 65 kutoka kata zote za wilaya ya bukombe walipatiwa mafunzo ya namna ya kumuandaa mwanafunzi ili ajue kusoma,kuhesabu na kuandika, lengo kuu likiwa ni kuboresha kiwango cha ufaulu katka Wilaya hiyo.Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo Afisa Elimu wa Mkoa aliwapongeza viongozi wa Wilaya hiyo kwa uamuzi wao wa kutoa mafunzo hayo ambayo yanamwezesha mwalimu kwenda na wakati katika utoaji wa elimu bora kwa wanafunzi ili kuendana na malengo ya matokeo makubwa sasa.