MAWASILIANO YA BLOG

KWA MAONI NA USHAURI WASILIANA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO KWA SIMU NAMBA 0764 143 977 AU E-MAIL: habarigeita@gmail.com

Tuesday 25 November 2014

Katibu Tawala Mpya Mkoa wa Geita Ndugu Charles Pallangyo akizungumza na watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Geita na Taasisi nyingine za Umma na mashirika ambao walihudhuria Sherehe za Makabidhiano ya Ofisi kati yake na aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa huu Ndugu Severine Kahitwa. Katika makabidhiano hayo ndugu Pallangyo aliwataka watumishi kuonyesha ushirikiano na kufanya kazi kwa bidii katika majukumu yao ya kila siku huku akiwaagiza wakuu wa idara zote kuhakikisha kuwa wanafanya vikao na watumishi kila mwezi na muhtasari wa vikao hivyo unawasilishwa kwake mapema iwezekanavyo.Aidha aliwaomba wadau wote wa maendeleo kutoa ushirikiano katika masuala ya maendeleo ya Mkoa huu pale watakapohitajika kufanya hivyo.