MAWASILIANO YA BLOG

KWA MAONI NA USHAURI WASILIANA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO KWA SIMU NAMBA 0764 143 977 AU E-MAIL: habarigeita@gmail.com

Wednesday 12 November 2014

MKUTANO WA TISA WA WADAU WA SEKTA NDOGO YA PAMBA WAFANYIKA MKOANI GEITA

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Geita Amani Mwenegoha akihutubia katika Mkutano wa wadau wa Sekta ndogo ya Pamba Mkoa wa Geita.Katika Mkutano huo ambao Mhe Amani alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa  Geita Mhe.Fatma Mwassa aliwapongeza kwa dhati viongozi wa Bodi ya Pamba kwa kushirikiana ta Tanzania Gastby Trust kwa kuendelea kuwezesha utaratibu wa wadau wa Pamba kukutana kila baada ya miezi mitatu uamuzi ambao utawanufaisha wakulima na Wafanyabiashara wa zao la Pamba Mkoa wa Geita.Mkutano huo ulikusudia kujadili kwa kina mkakati wa utekelezaji wa kilimo mkataba katika msimu 2014/2015, Mkakati wa kila halmashauri katika kuongeza uzalishaji wa Pamba kutoka kilo 400 kufikia kilo 800 kwa ekari.