MAWASILIANO YA BLOG

KWA MAONI NA USHAURI WASILIANA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO KWA SIMU NAMBA 0764 143 977 AU E-MAIL: habarigeita@gmail.com

Thursday 29 May 2014

BANKI YA NMB YA CHANGIA VIFAA SEKTA ZA AFYA NA ELIMU MKOA WA GEITA



 
Mkuu wa Mkoa wa GeitaMhe.Magalula Saidi akikabidhiwa madawati  na Meneja wa NMB kanda ya ziwa ndg. John Chilongola wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika viwanja vya Halmashauri ya Mji wa Geita.
Benki ya NMB Tawi la Geita Mkoani hapa imechangia vifaa vyenye thamani ya Tsh. 25 million katika Sekta ya Afya na Elimu.  Mchango huo unatokana na ahadi iliyotolewa na Benki hiyo wakati wa uzinduzi rasmi wa Mkoa wa Geita mnamo tarehe 08/11/2013 alisema Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita Bw. Severine Kahitwa alipokuwa akifungu hafla hiyo fupi.

Akizungumza katika makabidhiano hayo Meneja wa NMB Kanda ya Ziwa Ndugu John Chilongola alisema kuwa ni utaratibu wa Benki hiyo kutoa msaada katika jamii inayozungukwa na Benki hiyo ili kutatua changamoto zinazokabili jamii katika sekta ya elimu na afya.

Vifaa hivyo vilivyokabidhiwa vina thamani ya Tshs. 25million ambapo ni madawati 100 yenye thamani ya Tshs. 10mill, mashuka 500, vitanda viwili vya kujifungulia na vitanda 10 vya wagonjwa na magodoro yake.

Akizungumza baada ya kupokea vifaa hivyo Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Geita Magalula Said Magalula aliwapongeza sana viongozi wa Banki hiyo kwa kuona umuhimu wa kuusaidia Mkoa wa Geita katika sekta za Afya na Elimu kwani Mkoa una upungufu mkubwa sana wa madawati na vifaa vya Afya.

Aidha, alitoa wito kwa wananchi na wadau wengine wenye moyo kuendelea kutoa michango hiyo ya hali na mali ili kuweza kusaidia katika sekta mbalimbali ndani ya Mkoa na aliahidi kuwa vifaa hivyo vitatunzwa na kufikishwa katika maeneo husika.

Aliwaomba viongozi wa dini waliohudhuria hafla hiyo kutangaza matatizo yanazozikabili sekta mbalimali ili wananchi wahamasike  kuchangia huduma hizi muhimu.

Katibu Tawala Mkoa wa Geita alitoa maelekezo dhidi ya mgao wa vifaa hivyo katika Halmashari zote ambapo alieleza kuwa mashuka 100 yanakwenda kituo cha Afya Msumbwe Wiaya ya Mbogwe, mashua 100 yanakwenda kituo cha Afya Bwerwa Wilaya ya Mbogwe, mashuka 100 yanakwenda kituo cha Afya Kharumwah Wilaya ya Nyang’hwale, kituo cha Afya Kachwamba Wilayani Chato mashuka 50, kituo cha Afya Bulega mashuka 50 Wilaya ya Bukombe, Chikobe mashuka 50 na Kashishi mashuka 50 Wilaya ya Geita.

Madawati 100 yanakwenda katika shule ya msingi Nyanza iliyopo Kata ya Kalangalala ili kumaliza tatizo la madawati katika shule hiyo. Wakati vitanda viwili vya kujifungulia vinakwenda katika vituo vya Kharumwah na Iboya.

Msaada huu umekuja katika muda muafaka wakati Mkoa wa Geita ukiwa katika mkakati mkubwa wa kuboresha sekta za elimu na afya.

Na: Magesa  Jumapili.