MAWASILIANO YA BLOG

KWA MAONI NA USHAURI WASILIANA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO KWA SIMU NAMBA 0764 143 977 AU E-MAIL: habarigeita@gmail.com

Wednesday 15 October 2014

''MKOA WA GEITA NA JUHUDI ZA UHAMASISHAJI WA UFUGAJI WA SAMAKI''

Afisa Uvuvi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita ndugu Tito Mlelwa wakwanza kulia pamoja na wafugaji wa Samaki wakiwa wameshika Samaki ambao wametokana na Ufugaji ambao unahamasishwa na Uongozi wa Mkoa kwa lengo la kuongeza kipato na kuleta maendeleo katika kaya na Mkoa.                                                                                              Ufugaji wa Samaki ni shughuli muhimu ambayo inasaidia katika kukuza uchumi katika kaya na Taifa, kwa kutambua hilo Mkoa wa Geita unahamasishwa Ufugaji wa Samaki kama njia mojawapo ya kupambana na umaskini na ukosefu wa lishe bora kwa wananchi wake. Uhamasishaji huu unafanywa katika Wilaya zote tano (5) za Mkoa huu kupitia Idara ya Uchumi na uzalishaji. Mwaka 2013 kulikuwa na Mabwawa ya Samaki 33 kwa Mkoa mzima mpaka hivi sasa kuna jumla ya Mabwawa ya Samaki 92. Uhamasishaji wa kufuga Samaki unafanywa kwa wataalamu kuwatembelea wafugaji vijijini na kuwaeleza juu ya faida zitokanazo na Ufugaji wa Samaki pamoja na kuwapatia mbinu bora za Ufugaji wa Samaki.