MAWASILIANO YA BLOG

KWA MAONI NA USHAURI WASILIANA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO KWA SIMU NAMBA 0764 143 977 AU E-MAIL: habarigeita@gmail.com

Thursday 26 March 2015

Mhe. George Simbachawne Waziri wa Nishati na Madini akikagua shughuli za uchimbaji wa madini ya dhahabu katika Mdodi wa Busolwa Mine wakati wa Ziara yake Mkoa wa Geita.
Mwekezaji wa ndani ambaye pia ni mmiliki wa kampuni ya uchimbaji wa madini ya Busolwa Mine Baraka Ezekiel akimwelezea waziri namna shughuli za uchimbaji wa madini zinavyofanyika katika Mgodi huo wakati wa ziara ya Waziri wa Nishati na Madini Mkoa wa Geita. Kushoto kwa Mhe. Waziri ni mhe Fatma Mwassa Mkuu wa Mkoa wa Geita na Mhe.Agustino Maselle Mbunge wa Jimbo la Mbogwe Mkoa wa Geita.
Mhe. George Simbachawene Waziri wa Nishati na Madini akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa mgodi wa Busolwa Mine alipotembelea Mgodi huo Nyarugusu Mkoani Geita. Mstari wa Mbele waliokaa kutoka kilia  kwa Waziri wapili ni Agustino Maselle Mbunge wa Mbogwe, ndugu Charles Pallangyo Katibu Tawala Mkoa wa Geita na kushoto kwa waziri ni ndugu Baraka Ezekiel Meneja wa Busolwa Mine,Mhe.Fatma Mwassa Mkuu wa Mkoa Geita na Mhe. Manzie Mangochie Mkuu wa Wilaya ya Geita.