MAWASILIANO YA BLOG

KWA MAONI NA USHAURI WASILIANA NA OFISI YA HABARI NA MAWASILIANO KWA SIMU NAMBA 0764 143 977 AU E-MAIL: habarigeita@gmail.com

Thursday 26 March 2015

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI ATEMBELEA MKOA WA GEITA WANANCHI WATAKIWA KUSHIRIKIANA NA WAWEKEZAJI ILI KUJILETEA MAENDELEO NA KUKUZA UCHUMI WA NCHI.

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya uchimbaji madini ya Geita Gold Mine (GGML) Michael Van Anen akimkabidhi waziri wa Nishati na Madini hundi ya  tshs bilioni 2.23 kama ushuru wa tozo (service levy) kwa halmashauri  ya Geita na halmashauri ya Geita mjini wakati wa hafla hiyo iliyofanyika katika viwanja vya Halmashauri ya mji wa Geita na kuhudhuriwa na viongozi wa taasisi mbalimbali za serikali ,dini na binafsi.

Mhe. George Simbachawene Waziri wa Nishati na Madini akiwakabidhi hundi ya Tshs bilioni 2.23 wenyeviti wa Halmashauri ya Geita na Halmashauri ya Geita Mjini. Fedha hiyo inatokana na kodi ya ushuru wa tozo (service levy) iliyolipwa na kampuni ya uchimbaji wa madini ya Geita (GGML). Aliwataka Wenyeviti hao kuhakikisha kuwa fedha hizo zinafanya kazi za maendeleo na siyo vinginevyo ili kukuza uchumi na maendeleo ya Mkoa wa Geita. Hata hivyo aliwaeleza wananchi kuwa watarajie kuona huduma bora zaidi kwenye elimu, afya, barabara, umeme na maji. Kampuni ya GGM imekuwa ikisaidia katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Mkoa huu kama vile ujenzi wa shule,ujenzi wa nyumba za watumishi na kituo cha afya Nyakabale, maji na kituo cha ushauri nasaha Geita.